Ukame mkali umeacha zaidi ya Wakenya milioni mbili wakikabiliwa na njaa, huku jamii za wafugaji katika eneo la Kaskazini Mashariki zikionekana kuathirika zaidi
Idara hiyo imesema kuwa sehemu kubwa ya nchi itashuhudia joto kali hadi mvua zitakapoanza mwezi Machi.
Hata hivyo, hali ya ukame kuliko kawaida inatarajiwa katika maeneo ya pwani ya Kenya, hali inayohitaji tahadhari ya mapema kwa jamii na wadau wa sekta nyeti kama kilimo na maji.